Ripoti mpya ya robo mwaka kuhusu uchumi wa dunia ya shirika la Fedha Duniani, imeonesha ukuaji mdogo wa uchumi kidunia huku ikionya kuhusu vita vya kibiashara, uwezekano wa kukosekana kwa mkataba wa Brexit na changamoto nyingine zinazochangia kudorora kwa uchumi
Ripoti hiyo inasema kuwa mizozo ya kibiashara imepunguza kasi ya uwekezaji na kudorora kwa sekta ya viwanda na imetoa wito kwa mataifa kutotumia tozo kumaliza tofauti zao
Uchumi wa dunia umeendelea kukua kwa kasi ndogo ambapo katika mwaka 2019 uchumi wa unatarajiwa utakuwa kwa asilimia 3.2 na asilimia 3.5 kwa mwaka 2020
Aidha, shirika hilo limesema ikiwa hali ya sasa itaendelea kushuhudiwa mfululizo, basi huenda mambo yakawa mabaya zaidi kwa mataifa mengi na hasa yale yanayoendelea


No comments:
Post a Comment