Airtel

Airtel
Twanga kotekote

Monday, July 29, 2019

PAUL MAKONDA: WASIOFUA NGUO, KUNYOOSHA, KUOGA MARUFUKU DSM HADI MKUTANO WA SADC UMALIZIKE



Mkuu wa Mkoa wa Dar amepiga marufuku watu wachafu kuonekana maeneo ya katikati ya mji hasa wakati wa mkutano wa wakuu wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)

Makonda amesema kuja mjini bila kunyoosha nguo na kuoga ni marufuku. Wapo wanaotembea na chawa. Kama huwezi kuwa msafi basi subiri mkutano upite

Amesisitiza kuwa hataki kumtia aibu Rais Magufuli mbele ya Marais kutoka nchi 15 watakaokuwa hapa nchini

Ameyasema hayo leo wakati akizindua kampeni ya usafi ikiwa ni moja ya maandalizi ya mkutano wa 39 wa SADC unaotarajiwa kufanyika hapa nchini Agosti 17 na 18, 2019.

Waziri LUGOLA amtumbua RTO ARUSHA kutotii maagizo



Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amemuondoa madarakani Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani Mkoani Arusha (RTO), Charles Bukombe kwa madai ya kupuuza maagizo yake na kuyaita ya kisiasa

Taarifa ya Wizara hiyo imeeleza kuwa Waziri Lugola amemuagiza pia Katibu Mkuu wa wizara, kumchukulia hatua za kinidhamu Askari huyo ili iwe fundisho kwa wengine

Lugola amesema amemshuhudia Bukombe katika video inayosambaa mitandaoni alipokuwa katika mkutano jijini Arusha akipinga maagizo yake na kuyaita ya kisiasa na hakuyatekeleza


Aidha, akiwa katika mkutano wa hadhara katika mji wa Malinyi mkoani Morogoro jana, Lugola amesema hatoi maagizo ya kisiasa ila hutoa yanayomsaidia Rais Magufuli