Mkuu wa Mkoa wa Dar amepiga marufuku watu wachafu kuonekana maeneo ya katikati ya mji hasa wakati wa mkutano wa wakuu wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)
Makonda amesema kuja mjini bila kunyoosha nguo na kuoga ni marufuku. Wapo wanaotembea na chawa. Kama huwezi kuwa msafi basi subiri mkutano upite
Amesisitiza kuwa hataki kumtia aibu Rais Magufuli mbele ya Marais kutoka nchi 15 watakaokuwa hapa nchini
Ameyasema hayo leo wakati akizindua kampeni ya usafi ikiwa ni moja ya maandalizi ya mkutano wa 39 wa SADC unaotarajiwa kufanyika hapa nchini Agosti 17 na 18, 2019.

No comments:
Post a Comment