Airtel

Airtel
Twanga kotekote

Tuesday, January 19, 2021

Saa za Trump White House zayoyoma

 


Sherehe za kuapishwa kwa Rais Mteule wa Marekani, Joe Biden zinatarajiwa kufanyika kesho majira ya mchana kwa saa za Marekani.

Mwanamuziki Lady Gaga  anatarajiwa kuimba wimbo wa Taifa hilo katika hafla hiyo  ambayo inatarajiwa kuhudhuriwa na watu wachache.

Makamu wa Rais Kamala Harris ataapishwa kabla ya Biden  kuapishwa na kuhutubia.

Ulinzi umeimarishwa maradufu katika jiji la Washington DC ambapo maelfu ya askari wameongezwa katika jiji hilo.

Rais Mteule Biden  na Makamu wa Rais mteule Kamala  wanatarajiwa kuwasili jijini Washington  hii leo kwa ndege.

Aidha baadae leo ibada maalum inatarajiwa kufanyika kuwakumbuka maelfu ya watu waliofariki duniani  baada ya kuugua Corona nchini Marekani.

No comments:

Post a Comment